Thursday 28th, March 2024
@Nanyamba
Zoezi la kumezesha dawa za magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa shule za msingi, Halmashauri ya Mji Nanyamba yameanza leo Mei 8, 2018. Uzinduzi wa zoezi hilo umefanyika katika shule ya Msingi Dinyecha ambapo Afisa Muuguzi Mkuu wa Halmashauri Bi. Juliana Chikumba alimwakilisha Mkurugenzi wa Mji.
Afisa Muuguzi Mkuu wa Mji, Bi. Juliana Chikumba (Pichani) akizindua zoezi kwa kummezesha dawa mwanafunzi wa shule ya msingi Dinyecha mapema leo hii.
Aidha, Mratibu wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele wa Halmashauri Ndg. Mohamedi Tilika amezungumza na mwandishi wa habari wa Halmashauri ya Mji ambapo amesema, "Tunatarajia kulifanya zoezi hili kwa siku 3 kwa shule 65 za Msingi katika Halmashauri yetu, kuanzia leo Mei 8, huku tukitarajia kumezesha watoto 26,000 wa Shule za Msingi".
Walimu waliopata mafunzo ya utohaji huduma wakiwa wanamezesha wanafunzi dawa za magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele mapema hivi leo.
Alpipoulizwa kama kuna madhara yoyote ambayo yamejitokeza kwa watoto, Mratibu huyo ambaye kitaaluma ni Afisa Muuguzi Msaidizi alisema, "Hadi sasa hayajaripotiwa madhara yoyote ya dawa kwa watoto na bado tunaendelea kufanya kazi kwa karibu zaidi ili kuweza kujua kama kuna mtoto amedhurika".
Zoezi hili linakuja siku chache baada ya uendeshaji wa mafunzo ya utohaji huduma ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kufanyika kwa watoa huduma wa vituo vya afya pamoja na walimu wa shule za msingi Nanyamba.
NANYAMBA, MTWARA.
Sanduku la Barua: P.O.BOX 1490,
Simu: +255
Simu:
Barua pepe: td@nanyambatc.go.tz
Copyright ©2016 Nanyambatc . All rights reserved.