Mapema hivi leo Timu ya Lishe ya Halmashauri ya Mji Nanyamba ikishirikiana na Maafisa Lishe kutoka Wilaya ya Tandahimba imeweza kutembelea baadhi ya Vijiji viliovyopo Halmashauri ya Mji Nanyamba na kufanya utafiti wa lishe kwa Watoto kuanzia Miezi 0 mpaka miezi 59 katika kata ya Mtimbwilimbi na Mtiniko ili kuweza kujionea hali ya lishe kwa Watoto waliopo katika kata hizo. Timu imeweza kuchunguza maswala mbalimbali ya lishe ikiwa ni pamoja na
= Udumavu,
= Ukondefu na
= Uzito pungufu kwa Watoto.
Zoezi hili muhimu limenza rasmi leo tarehe 9/6/2025 na litadumu mpaka tarehe 18/6/2025 ambapo kata zote 17 zilizopo katika Halmashauri ya Mji Nanyamba zitafikiwa. Lengo likiwa na kupanga na kuboresha afua mbalimbali za lishe kutokana na matokeo ya utafiti huo
Hivyo basi wazazi na walezi wa watoto wenye umri wa miezi 0 mpaka miezi 59 mnahimizwa kuwaleta watoto wenu katika kila kituo kitakachoanishwa kwa kila kijiji na kata husika
NANYAMBA, MTWARA.
Sanduku la Barua: P.O.BOX 1490,
Simu: +255
Simu:
Barua pepe: td@nanyambatc.go.tz
Copyright ©2016 Nanyambatc . All rights reserved.