• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
NANYAMBA TOWN COUNCIL
NANYAMBA TOWN COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Nanyamba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya MSM
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
        • katiba
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ununuzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliagi na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Fedha na Biashara
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Mazingira na Usafi
      • Afya
      • Ujenzi
      • Maji
      • Elimu
        • Elimu Msingi
        • Elimu Sekondari
        • Michezo na Burudani
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Sheria
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba
      • Maktaba ya picha
      • Maktaba ya video
    • Habari
    • Matukio

WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA NIDHAMU.

Posted on: March 6th, 2018

WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA NIDHAMU.

Watumishi wa umma Halmashauri ya Mji Nanyamba wametakiwa kufanya kazi kwa weledi na nidhamu katika kutekeleza majukumu yao wanapowahudumia wananchi.
Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Mji, Advoc. Oscar Ng’itu alipokuwa akifungua mafunzo elekezi ya awali kwa watumishi wapya wa umma walioajiliwa katika Halmashauri ya Mji Nanyamba, mafunzo yalifanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Kutwa Nanyamba Machi 5, 2018.

Mkurugenzi alisema kuwa msingi wa utumishi wa umma umejikita katika uadilifu, hivyo mtumishi wa umma lazima afanye kazi kwa weledi na nidhamu ya hali ya juu. Aliongeza kuwa Utumishi wa umma huendeshwa kwa misingi yake, Ofisi za Umma haziendeshwi kama tunavyoendesha familia zetu, ni ofisi ambayo ina misingi na miongozo huku akiwasisitiza watumishi wakatoe huduma kwa wananchi bila kuwabagua.

Akiongelea umuhimu wa mafunzo elekezi ya awali kwa watumishi wa umma, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji alisema kuwa watumishi wengi wanatoka katika maeneo tofauti yenye mitazamo tofauti hivyo, kuhitaji kufundishwa utaratibu wa kazi katika serikali. “Mafunzo haya ni muhimu sana unapoingia katika utumishi wa umma. Tunatoka katika maeneo tofauti na tamaduni tofauti hivyo, hata tabia zinakuwa tofauti. Mafunzo haya yanalenga kutufundisha namna utumishi wa umma ulivyo na jinsi mtumishi wa umma anavyotakiwa kuonekana na kutenda kazi” alisema Mkurugenzi.

Aliwataka watumishi hao kubadilika baada ya mafunzo kimtazamo na kiutendaji na kuzingatia viwango vya juu katika utumishi wao “Mnatakiwa mjue nafasi zenu mlizonazo. Sasa msiniangushe, Utawala tulionao ni utawala ambao unapenda kero zianze kukatuliwa kuanzia chini. Mimi siku hizi akija mwananchi ofisini kwangu nitaanza kumuuliza kama amepita kwanza kwako ili tupunguze ile kasi ya wananchi kuja Halmashauri. Huko vijijini kuna timu; afisa ugani, daktari, mratibu elimu, mwalimu mkuu, mkuu wa shule; hawa wote wanatakiwa wawajibike kwako. Kuna changamoto mkienda vijijini kila mmoja anapita njia zake mnakosa kushirikiana kiasi kwamba mnakosa kuwa na lugha moja”.

Aidha, Mkurugenzi aliwataka watumishi wakaishi vijijini kama wananchi wanavyoishi bila kuwabagua. “Sisi sote ni watanzania, yawezekana wengine mnatoka familia bora lakini mazingira ya vijijini unatakiwa kuishi kama wananchi wanavyoishi, msiende huko mkawabagua watu. Muende mkawahudumie wananchi kama ambavyo kanuni na taratibu zinavyotuongoza”. Alisema Mkurugenzi.

Katika Mafunzo hayo, watumishi wa umma wapya walielekezwa mambo mbalimbali yahusuyo Utumishi wa Umma yakiwemo Kanuni na Maadili ya Utumishi wa Umma, Haki na wajibu wa mwajiri na mwajiriwa, Mahusiano kazini, Ukusanyaji mapato, Kazi za kamati za Halmashauri za vijiji, uandishi wa mihutasari ya vikao, uendeshaji wa vikao kwa ngazi ya kata na vijiji na mengineyo.

Mafunzo elekezi ya awali kwa watumishi wapya wa umma yameandaliwa na ofisi ya Mkurugenzi wa Mji Nanyamba kupitia Idara na Vitengo yakishirikisha watumishi wapya 48.

Matangazo

  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA July 02, 2024
  • Fungua zote

Habari Mpya

  • TANGAZO KWA WANANANYAMBA

    June 02, 2025
  • TAFITI YA LISHE YAENDELA KWA KASI HALMASHAURI YA MJI NANYAMBA

    June 13, 2025
  • RC SAWALA AFURAHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    June 10, 2025
  • TAFITI YA LISHE KWA WATOTO KUANZIA MIEZI 0 HADI MIEZI 59

    June 09, 2025
  • Fungua zote

Video

Video zinginezo

Kurasa za karibu

  • Kupata Salary slip
  • Renovation of 17 AMREF Water Projects
  • Uuzaji wa Viwanja
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KATIKA SHULE MBALIMBALI ZA SEKONDARI-HALMASHAURI YA MJI NANYAMBA 2022/2023
  • YOUTUBE; Nanyamba town council
  • INSTAGRAM; nanyambatc3
  • FACEBOOK; Nanyamba Town Council
  • TWITTER/ X; nanyambatc1

Kurasa Mashuhuri

  • Government Portal
  • PO - RAG
  • State House Website
  • Public Services Recruitment Secretariet
  • Tanzania Government Portal
  • Public Services Website

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahala

Wasiliana nasi

    NANYAMBA, MTWARA.

    Sanduku la Barua: P.O.BOX 1490,

    Simu: +255

    Simu:

    Barua pepe: td@nanyambatc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2016 Nanyambatc . All rights reserved.