Mhe. Abdallah Dadi Chikota (Mb) ametembelea miradi mbalimbali ya maendeleo inayoendelea katika Halmashauri ya mji Nanyamba na kufanya mikutano ya hadhara kwa wananchi siku ya Jumatano tarehe 05/07/2023. Katika ziara hiyo Mhe. Chikota amewahimiza wananchi kutumia fursa mbalimbali zinazojikokeza katika Halmashauri hiyo zikiwemo ujenzi wa barabara, shule za msingi na sekondari katika kujiletea maendeleo ya kiuchumi.
Miradi iliyotembelewa na kukaguliwa ni pamoja mradi wa ujenzi unaondelea katika shule ya sekondari ya Dinyecha ambapo ipo katika hatua ya boma huku akionesha kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa mradi huo. Pia ameahidi kuongeza mifuko 50 ya saruji itakayotumika kumalizia ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Chikwaya pamoja na nyumba ya mganga mkuu.
Aidha, Mhe. Chikota amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuteua Halmashauri ya Mji Nanyamba kufanya ubanguaji wa korosho kitaifa, ambapo tayari eneo la Maranje limetengwa kwaajili ya ujenzi wa viwanda vya kubangua korosho na kukamua mafuta kwenye Maganda ya korosho.
NANYAMBA, MTWARA.
Sanduku la Barua: P.O.BOX 1490,
Simu: +255
Simu:
Barua pepe: td@nanyambatc.go.tz
Copyright ©2016 Nanyambatc . All rights reserved.