BARAZA LA WAZEE LA HALMASHAURI YA MJI NANYAMBA LAZINDULIWA RASMI
Leo tarehe 23.12.2020 Mkuu wa wilaya ya Mtwara Mh. Danstun Kyobya amelizindua rasmi baraza la wazee la Halmashauri
ya Mji wa Nanyamba ambalo litawakilisha wazee wa Halmashauri ya Mji nanyamba kwenye baraza la wazee la Mkoa wa Mtwara
, baraza hilo linalosimamiwa na Mganga mkuu wa Halmashauri ya Mji Nanyamba kwa niaba ya Mkurugnzi wa Mji linaundwa
na wajumbe kutoka katika kata zote 17 za Halmashauri ya Mji Nanyamba.
Pamoja na mambo mengine baraza hilo lilichagua uongozi kwa nafasi za mwenyekiti, makamu mwenyekiti, katibu,
katibu msaidizi, mtunza hazina na wawakilishi wawili( wa kike na wa kiume) kama ifuatavyo:
1. Mwenyekiti- Salim Saidi Namtumbikanya
2. Makamu mwenyekiti- Mohamedi Ismaili Adilike
3. Katibu- Mwang'aka Mohamedi Ally
4. Katibu Msaidizi- Kalauka Abdalah Hamisi
5. Mtunza Hazina-
6. Mwakilishi Wanaume-
7. Mwakilishi Wanawake-
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Nanyamba Ndugu Thomas Mwailafu aliwaagiza viongozi waliochaguliwa kutimiza majukumu yao
kwa kadri ya miongozo na kanuni za Baraza la wazee ili waweze kuwasaidia wazee wote wa Halmashauri ya Mji wa Nanyamba
kutambulika na kupata haki zao.
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Mtwara Mh. Danstun kyobya alimuagiza mganga mkuu wa Halmashuri ya mji ahakikishe
wazee wanahamasishwa kujiunga na bima ya jamii ya afya lakini pia wanapewa kipaumbelea katika vituo vya kutolea huduma
za afya kwani wazee ni hazina ya Taifa.
NANYAMBA, MTWARA.
Sanduku la Barua: P.O.BOX 1490,
Simu: +255
Simu:
Barua pepe: td@nanyambatc.go.tz
Copyright ©2016 Nanyambatc . All rights reserved.